Artwork

Вміст надано Iran.Tanzania. Весь вміст подкастів, включаючи епізоди, графіку та описи подкастів, завантажується та надається безпосередньо компанією Iran.Tanzania або його партнером по платформі подкастів. Якщо ви вважаєте, що хтось використовує ваш захищений авторським правом твір без вашого дозволу, ви можете виконати процедуру, описану тут https://uk.player.fm/legal.
Player FM - додаток Podcast
Переходьте в офлайн за допомогою програми Player FM !

Qasem

10:07
 
Поширити
 

Manage episode 337502596 series 3382153
Вміст надано Iran.Tanzania. Весь вміст подкастів, включаючи епізоди, графіку та описи подкастів, завантажується та надається безпосередньо компанією Iran.Tanzania або його партнером по платформі подкастів. Якщо ви вважаєте, що хтось використовує ваш захищений авторським правом твір без вашого дозволу, ви можете виконати процедуру, описану тут https://uk.player.fm/legal.

MIAKA MIWILI YA KUMBUKIZI YA KIFO CHA LUTENI JENERALI QASSEM SOLEIMANI

Usiku wa manane wa kuamkia Ijumaa 3 Januari Mwaka 2020, wakati anga ya jiji la Baghdad mji mkuu wa Iraq ikiwa tulivu, ghafla watu wa mji huo walishtushwa na kuamshwa na milio ya milipuko na kuwafanya waingiwe na taharuki wakidhani kuwa kundi la kigaidi la ISIS limeushambulia tena mji huo. Baada ya masaa machache, zilianza kusambaa taarifa za kuuawa Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran IRGC, ambaye alienda nchini Iraq kwa mwaliko rasmi wa viongozi wa nchi hiyo, akiwa pamoja na Naibu Mkuu wa Harakati ya Al-Hashdu al-Sha’abi Abu Mahdi Al-Muhandis na wengine wanane waliuliwa shahidi baada ya msafara wa magari yaliyowabeba kulengwa na kushambuliwa na makombora ya majeshi ya Marekani karibu na uwanja wa ndege wa Baghdad, mji mkuu wa nchi hiyo.

Kamanda Soleimani ambaye amepewa lakabu ya bwana wa mashahidi wa muqawama, katika umri wake wote uliojaa baraka na akiwa kamanda wa IRGC, alikuwa mstari wa mbele kuyasaidia na kuyaunga mkono mataifa yote yanayodhulumiwa ya Waislamu, bila ya kujali ni mataifa ya watu gani. Muhimu kwake muda wote ilikuwa ni kupigania Uislamu na mafundisho sahihi ya Qur'ani Tukufu.

Shujaa huyu (Qassem Soleimani) alizaliwa tarehe 11 Machi 1957, katika kijiji cha Qanat-e Malek, Mkoa wa Kerman nchini Iran. Wakati wa harakati za mapinduzi ya Kiislamu zikiwa zimepamba moto, Qassem Soleimani alifahamiana na mwanachuoni mmoja wa kidini aliyeitwa Sheikh Reza Kamyab aliyetoka mji wa Mashhad, ulioko kaskazini mashariki mwa Iran na kwenda mjini Kerman kulingania dini, sanjari na kuelezea dhulma na ukandamizaji unaofanywa na utawala wa kifalme dhidi ya wananchi wa matabaka mbalimbali nchini humo. Qassim Soleimani alivutiwa mno na hotuba za mwanachuoni huyo zenye kuhamasisha wananchi kujitolea na kupambana na utawala wa kitaghuti uliokuwa ukitawala nchini humo. Baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (1979), Soleimani alijiunga na Kikosi cha Kulinda Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC).

Mnamo mwaka 1998, Kamanda Soleimani aliteuliwa na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi yote nchini, kuwa kamanda wa Brigedi ya Quds. Katika jukumu hilo, kamanda Soleimani aliweza kuimarisha satua na ushawishi wa Iran katika eneo la magharibi mwa Asia, na hasa katika suala la kuleta mwamko wa Kiislamu na kuimarisha zaidi harakati ya Hizbullah nchini Lebanon na makundi mengine ya muqawama huko Palestina.

Akiwa Mkuu wa Kikosi cha Quds, Luteni Jenerali Qassem Soleimani alifanikiwa kuliangamiza genge la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) katika nchi mbili za Kiarabu za Iraq na Syria na pia alifanikiwa kuwapa zawadi ya amani, utulivu na usalama wananchi wa nchi hizo mbili, kwa kuasisi kwake harakati za kujitolea za wananchi.

Qassem Suleimani alipewa majukumu mbalimbali ndani na nje ya nchi, yakiwemo ya kupatanisha migogoro ya wenyewe kwa wenyewe katika nchi rafiki, na ukiwemo mgogoro ulioibuka kati ya jeshi la Iraq na kikosi cha wanamgambo wa Mahdi nchini humo, mwezi Machi 2008.

Mnamo tarehe 24 Januari 2011, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Sayyed Ali Khamenei na Amiri Jeshi Mkuu, alimpandisha cheo kamanda Qassem Soleimani, na kuwa Meja Jenerali. Ayatullah Khamenei alikuwa na uhusiano wa karibu mno na kamanda Soleimani na kufikia hatua ya kumuita "shahidi aliye hai". Mnamo Machi 2019, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu alimtunuku kamanda Qassem Soleimani nishani ya "Dhul Faqar", na kumfanya kuwa kamanda wa kwanza wa kijeshi kupokea heshima hiyo, tangu ulipopatikana ushindi wa mapinduzi ya Kiislamu ya Iran mwaka 1979.

--- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message
  continue reading

12 епізодів

Artwork

Qasem

Iran-Tanzania Podcast

published

iconПоширити
 
Manage episode 337502596 series 3382153
Вміст надано Iran.Tanzania. Весь вміст подкастів, включаючи епізоди, графіку та описи подкастів, завантажується та надається безпосередньо компанією Iran.Tanzania або його партнером по платформі подкастів. Якщо ви вважаєте, що хтось використовує ваш захищений авторським правом твір без вашого дозволу, ви можете виконати процедуру, описану тут https://uk.player.fm/legal.

MIAKA MIWILI YA KUMBUKIZI YA KIFO CHA LUTENI JENERALI QASSEM SOLEIMANI

Usiku wa manane wa kuamkia Ijumaa 3 Januari Mwaka 2020, wakati anga ya jiji la Baghdad mji mkuu wa Iraq ikiwa tulivu, ghafla watu wa mji huo walishtushwa na kuamshwa na milio ya milipuko na kuwafanya waingiwe na taharuki wakidhani kuwa kundi la kigaidi la ISIS limeushambulia tena mji huo. Baada ya masaa machache, zilianza kusambaa taarifa za kuuawa Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran IRGC, ambaye alienda nchini Iraq kwa mwaliko rasmi wa viongozi wa nchi hiyo, akiwa pamoja na Naibu Mkuu wa Harakati ya Al-Hashdu al-Sha’abi Abu Mahdi Al-Muhandis na wengine wanane waliuliwa shahidi baada ya msafara wa magari yaliyowabeba kulengwa na kushambuliwa na makombora ya majeshi ya Marekani karibu na uwanja wa ndege wa Baghdad, mji mkuu wa nchi hiyo.

Kamanda Soleimani ambaye amepewa lakabu ya bwana wa mashahidi wa muqawama, katika umri wake wote uliojaa baraka na akiwa kamanda wa IRGC, alikuwa mstari wa mbele kuyasaidia na kuyaunga mkono mataifa yote yanayodhulumiwa ya Waislamu, bila ya kujali ni mataifa ya watu gani. Muhimu kwake muda wote ilikuwa ni kupigania Uislamu na mafundisho sahihi ya Qur'ani Tukufu.

Shujaa huyu (Qassem Soleimani) alizaliwa tarehe 11 Machi 1957, katika kijiji cha Qanat-e Malek, Mkoa wa Kerman nchini Iran. Wakati wa harakati za mapinduzi ya Kiislamu zikiwa zimepamba moto, Qassem Soleimani alifahamiana na mwanachuoni mmoja wa kidini aliyeitwa Sheikh Reza Kamyab aliyetoka mji wa Mashhad, ulioko kaskazini mashariki mwa Iran na kwenda mjini Kerman kulingania dini, sanjari na kuelezea dhulma na ukandamizaji unaofanywa na utawala wa kifalme dhidi ya wananchi wa matabaka mbalimbali nchini humo. Qassim Soleimani alivutiwa mno na hotuba za mwanachuoni huyo zenye kuhamasisha wananchi kujitolea na kupambana na utawala wa kitaghuti uliokuwa ukitawala nchini humo. Baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (1979), Soleimani alijiunga na Kikosi cha Kulinda Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC).

Mnamo mwaka 1998, Kamanda Soleimani aliteuliwa na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi yote nchini, kuwa kamanda wa Brigedi ya Quds. Katika jukumu hilo, kamanda Soleimani aliweza kuimarisha satua na ushawishi wa Iran katika eneo la magharibi mwa Asia, na hasa katika suala la kuleta mwamko wa Kiislamu na kuimarisha zaidi harakati ya Hizbullah nchini Lebanon na makundi mengine ya muqawama huko Palestina.

Akiwa Mkuu wa Kikosi cha Quds, Luteni Jenerali Qassem Soleimani alifanikiwa kuliangamiza genge la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) katika nchi mbili za Kiarabu za Iraq na Syria na pia alifanikiwa kuwapa zawadi ya amani, utulivu na usalama wananchi wa nchi hizo mbili, kwa kuasisi kwake harakati za kujitolea za wananchi.

Qassem Suleimani alipewa majukumu mbalimbali ndani na nje ya nchi, yakiwemo ya kupatanisha migogoro ya wenyewe kwa wenyewe katika nchi rafiki, na ukiwemo mgogoro ulioibuka kati ya jeshi la Iraq na kikosi cha wanamgambo wa Mahdi nchini humo, mwezi Machi 2008.

Mnamo tarehe 24 Januari 2011, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Sayyed Ali Khamenei na Amiri Jeshi Mkuu, alimpandisha cheo kamanda Qassem Soleimani, na kuwa Meja Jenerali. Ayatullah Khamenei alikuwa na uhusiano wa karibu mno na kamanda Soleimani na kufikia hatua ya kumuita "shahidi aliye hai". Mnamo Machi 2019, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu alimtunuku kamanda Qassem Soleimani nishani ya "Dhul Faqar", na kumfanya kuwa kamanda wa kwanza wa kijeshi kupokea heshima hiyo, tangu ulipopatikana ushindi wa mapinduzi ya Kiislamu ya Iran mwaka 1979.

--- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message
  continue reading

12 епізодів

所有剧集

×
 
Loading …

Ласкаво просимо до Player FM!

Player FM сканує Інтернет для отримання високоякісних подкастів, щоб ви могли насолоджуватися ними зараз. Це найкращий додаток для подкастів, який працює на Android, iPhone і веб-сторінці. Реєстрація для синхронізації підписок між пристроями.

 

Короткий довідник